MPIGIE KURA ANGEL KILIMUSIC AWARDS

Social Icons

Saturday, 9 February 2013

LULU KUFANYA 'PRESS CONFERENCE'

Baada ya watu wengi kuwa na shauku ya kuona na kujua ataongea nini muigizaji Elizabeth Michael a.k.a Lulu baada ya kutoka jela kwa dhamana kwenye kesi aliyokuwa nayo. Hatimaye bongomovie imepata habari za uhakika kutoka kwa mtu aliyehusika karibu zaidi na Lulu tangu akiwa anaanza kwenye uigizaji hadi alivyokuwa mahabusu kwenye kwa kesi yake na hadi kutoka. Sio mwingine bali ni Doctor Cheni, 

bongomovie ilikutana na Cheni live na kupiganaye story kadhaa likiwe la kumhusu Lulu. Kubwa zaidi ilikuwa kama ifuatavyo, “Watu au media nyingi zinataka kufanya mahojiano na Lulu, hakuna anayejua nia ya mtu yoyote kwa sasa. Hataweza kwenda kilam media na kuzungumza na kila mwandishi, ukizingatia mazingira haliyotoka na umri wake anahitaji kupumzika sana, lakini ni kwamba tutafanya press conference hivi karibuni na mambo kadhaa tutayazungumza. Kwasababu mchakato wa kesi haujaisha kila kitu lazima kiennde kwa utaratibu. Siwezi kukwambia ni siku gani kwasababu inaitaji arrangement ilitufanye hiyo press conference. Kama tunavyoongea hapa nitakujulisha lini tunafanya baada ya muda mfupi na watanzania wasome kupitia hapa.” - Dr Cheni